Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Janga la Corona:Tanzania yazuia safari za ndege kimataifa
AfyaHabari Mchanganyiko

Janga la Corona:Tanzania yazuia safari za ndege kimataifa

Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TCAA), imefuta safari za ndege za abiria za kimataifa, huku ikiweziwekea masharti ndege za mizigo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Zuio hilo limetolewa na TCAA jana tarehe 11 Aprili 2020, huku ikieleza sababu zake kuwa ni kudhibiti kasi ya ueneneaji Ugonjwa wa Homa Kali ya Mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (COVID-19).

Kwa mujibu wa taarifa ya TCAA, zuio hilo litadumu hadi mamlaka hiyo itakapotoa taarifa zaidi.

“Kutokana na janga la COVID-19, vikwazo vifuatavyo vimechukuliwa kuanzia Aprili 11 2020 hadi taarifa zaidi itakapotolewa. Ratiba zote za safari za kimataifa zimesitishwa,” inaeleza taarifa ya TCAA.

TCAA imeeleza kuwa, ndege za mizigo zitaruhusiwa kufanya safari, lakini zitapaswa kuwa na watu wachache ambao watawekwa karantini na serikali,  kwa gharama zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!