Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jamii yashauriwa usimamizi shirikishi wa misitu
Habari Mchanganyiko

Jamii yashauriwa usimamizi shirikishi wa misitu

Spread the love

JAMII imeshauriwa kuzingatia dhana ya usimamizi shirikishi wa misitu kibiashara yenye kulenga kuwapatia kipato kufuatia utunzaji wa misitu na uvunaji endelevu. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Afisa wa Kujenga Uwezo kutoka Shirika la Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG), Simon Lugazo amesema hayo kwenye mkutano wa madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mvomero, wakati umefika kwa jamii kutambua umuhimu wa kujenga mfumo mzuri wa kuhakikisha mapato yanaleta faida kwenye halmashauri zao.

Amesema usimamizi wa misitu kibiashara unawezekana kama kijiji kikiwa na mipango ukiwemo wa matumizi bora ya ardhi uliopitishwa katika ngazi zote.

Ametaja mpango mwingine kuwa ni mpango wa uvunaji wa msitu husika, mpango wa usimamizi wa msitu uliopitishwa ngazi ya kijiji halmashauri na sheria ndogo za usimamizi wa misitu zilizopitishwa ngazi ya kijiji na halmashauri.

Lugazo ameishauri jamii inayojihusisha na masuala ya uvunaji misitu katika kunufaika na usimamizi wa misitu kibiashara lazima ufuate njia endelevu za uhifadhi ili uvunaji ulete faida bila kuwa na matokeo hasi kwenye mazingira.

Lugazo amesema mauzo ya hewa ukaa na malipo kwa makampuni yanayotumia maji yanayotoka msituni mfano TANESCO na idara ya maji yanapaswa kuzingatiwa na kwamba sekta hizo zilipaswa kulipa asilimia 2 kwa watunzaji misitu.

Afisa huyo wa TFCG, alitolea mfano Halmashauri za wilaya ya Kilwa mkoani Lindi na Tunduru mkoani Ruvuma ambazo zimenufaika kwa kukusanya kiasi cha sh bil 1.4 kutokana na uvunaji endelevu wa mbao ambao ulifaidisha watu wapatao 33,868.

Pia amesema matumizi ya teknolojia bora inayozalisha mazao ya kutosha inapaswa kutumika ikiwemo ya kupanga kuni kwa ajili ya kupata mkaa kitaalamu kwa njia inayopendezwa na wajasiliamali na wanamazingira.

Lugazo amesema maeneo yaliyosimamiwa vizuri yakitoa mapato na asilimia 10 ikarudishwa halmashauri itasaidia kuboresha miradi mingine ikiwemo ujenzi wa madarasa kwenye vijiji husika huku pesa iliyokusudiwa ikaenda kwenye mambo mengine.

Naye Diwani wa kata ya Homboza Nelson Joseph ameushukuru mradi huo kwa kutoa elimu inayoonesha kuwa jamii nayo inaweza kunufaika na misitu baada ya kusimamia.

Joseph amesema kuwa awali jamii ilikuwa ikijitahidi katika kuhifadhi misitu lakini wamekuwa hawapati faida yoyote jambo ambalo limekuwa likiwakatisha tamaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!