Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jaji aliyejiuzulu afariki
Habari MchanganyikoTangulizi

Jaji aliyejiuzulu afariki

Jaji Mohamed Chande Othman akimpa mkono wa pole aliyekuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Jaji Upendo H. Msuya enzi za uhai wake alipofiwa na mwanaye
Spread the love

ALIYEKUWA  Jaji wa Mahakama Kuu, Upendo Msuya, amefariki dunia  leo Julai 19 katika hospitali ya Kairuki jijini Dar es Salaam, alipokuwa amelazwa baada ya kuugua kwa muda mrefu, anaandika Hamisi Mguta.

Taarifa za awali kutoka ndani ya familia zinaeleza kwamba marehemu amefariki kwa ugonjwa wa kiharusi na kwamba alikuwa amepelekwa hospitali na kurudishwa nyumbani kwa zaidi ya miezi mitatu.

Mei 15 Marehemu Upendo aliacha rasmi kazi ya ujaji baada ya rais Magufuli kuridhia ombi lake hilo ambapo ombi hilo lilikubaliwa pamoja na Aloysius Mujulizi, aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya kurekebisha Sheria Tanzania na Meck Sadick, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Ikumbukwe kuwa kifo kimemfika Upendo ikiwa ni miezi miwili tangu aache kazi ya ujaji.
Tutaendelea kukujulisha zaidi kuhusu utaratibu wa mazishi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

error: Content is protected !!