NCHI ya Irani imejibu tishio la Rais wa Marekani, Donald Trump kwa kumuonya kwamba atapoteza kila anachomiliki iwapo ataruhusu nchi yake kulishambulia Taifa hilo. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Mnamo terehe 23 Julai, 2018 kupitia akaunti yake ya Twitter, Rais Trump aliitaka Iran kutotishia taifa lake na kwamba ikifanya hivyo ataiangamiza kupitia vita.
Kamanda wa Kikosi Maalumu cha Iran, Meja Jenerali Qassem Soleiman amesema iwapo Trump ataanzisha vita dhidi ya nchi yake, vita hiyo itaharibu kila anachokimiliki.
Jenerali amemuonya Trump kwamba Jeshi la Iran lina nguvu na uwezo, pia liko tayari kumfikia popote alipo, huku akiapa kuwa iwapo Rais huyo wa marekani ataanzisha vita wako tayari kuimaliza.
Chanzo: BBC Swahili.
Leave a comment