Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Iran yagomea vikwazo vya Marekani
Kimataifa

Iran yagomea vikwazo vya Marekani

Rais wa Iran, Hassan Rouhani na Donald Trump wa Marekani
Spread the love

RAIS wa Iran, Hassan Rouhani ameahidi kupinga vikwazo vya Marekani dhidi ya taifa lake, vinavyotarajiwa kuanza kutekelezwa leo tarehe 5 Novemba 2018. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Mwishoni mwa wiki iliyopita Marekani ilitangaza kuibua vikwazo vya zamani na kuanzisha vikwazo vipya dhidi ya Iran, huku vikwazo hivyo vikilenga sekta ya taasisi za kifedha, mafuta, gesi, usafirishaji wa majini.

Akihutubia baraza la mawaziri la Iran leo Jumatatu, Rais Rouhani amesema Iran imetengeza sera za kufuta vikwazo vya Marekani.

Amelitaka baraza hilo kuhakikisha kwamba Marekani inaelewa kwa lugha rahisi kwamba, hawawezi kushughulika na taifa lao kwa kutumia nguvu, shinikizo na vikwazo.

Rouhani amejigamba kuwa, kitendo cha Marekani kuziondoa nchi nane zinazonunua mafuta ya Iran katika vikwazo vyake, ni ushindi kwa taifa lake.

“Jamhuri ya Kiislam ya Iran inaweza kuuza mafuta yake hata kama nchi nane hazijaondolewa kwenye vikwazo,” amesema Rouhani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!