Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ingizeni wake zenu – Zungu
Habari za Siasa

Ingizeni wake zenu – Zungu

Mussa Zungu, Mbunge wa Ilala
Spread the love

MUSSA Zungu, Mbunge wa Ilala, amewataka maofisa na askari magereza kulinda heshima ya nyumba za serikali waliokabidhiwa, kwa kuhakikisha wanaingiza wake zao. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya majengo 12 ya nyumba za askari hao zilizoko Ukonga, jijini Dar es Salaam leo tarehe 23 Januari 2020, Zungu amewataka kuingiza wake zao kwenye nyumba hizo.

Zungu amesema, nyumba hizo zimeombewa dua na mashekhe, mapadri pamoja na maaskofu, hivyo wanatakiwa kuwa waadilifu katika matumizi ya nyumba hizo.

“Nyumba hizi zimeombewa dua na masheikh na baba paroko. Na mtu atakayeingia kwenye nyumba hizi, dua hii ina maana muwe waadilifu. Mkiingia humu ndani ingizeni wake zenu ili kuwe na heshima kwa aliyejenga aliyetoa pesa na heshima ya kiti cha uraisi,” amesema Zungu.

Majengo hayo  anayokabidhiwa Rais John Magufuli,  majengo manne ni ya maafisa wa jeshi la magereza na nane kwa ajili ya maaskari wa kawaida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!