Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko India wapiga marufuku kuacha mke
Habari Mchanganyiko

India wapiga marufuku kuacha mke

Spread the love

SERIKALI ya India imeanza utekelezaji wa muswada wa sheria ya ulinzi wa haki katika Ndoa wa mwaka 2017 uliokwama kupitishwa na bunge la nchi hiyo, ambao unalenga kuwabana wanaume wa kiislamu kutoa talaka tatu. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Muswada huo ambao unatafisri utolewaji wa talaka tatu za papo kwa papo kama kosa la jinai ambapo mhusika anaweza kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela, ulikwama kupitishwa bungeni mwezi Agosti 2018 baada ya pande zote mbili (upinzani na serikali) kukosa makubaliano.

Muswada huo uliowasilishwa bungeni na serikali ya Narendra Modi ulikwama kupitishwa kutokana na kutopigiwa kura na wabunge wengi.

Akizungumza na wanahabari jana Waziri wa Sheria India, Ravi Shankar Prasad alisema serikali ya nchi hiyo imeamua kuanza utekelezaji wa sheria hiyo baada ya kukithiri kwa matukio ya utolewaji wa talaka hizo licha ya maamuzi yaliyotolewa na mahakama kuu ya nchi hiyo kuhusu usitishaji wa talaka hizo kutokana na kuwa kinyume na katiba ya India.

Hata hivyo, Vyama vya Upinzani India vimekosoa vikali uamuzi huo vikidai kuwa, baadhi ya masharti yaliyomo katika muswada huo ni magumu kutekelezeka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!