Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko IGP Sirro apangua makamanda wa mikoa
Habari Mchanganyiko

IGP Sirro apangua makamanda wa mikoa

Spread the love

MKUU wa jeshi la polisi nchini (IGP), Simon Sirro, ametangaza mabadiliko ya makamanda wa mikoa katika jeshi lake kwa kuhamisha baadhi huku na kupeleka kule. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Miongoni mwa waliohamishwa, ni pamoja na aliyekuwa Kamanda wa polisi mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishena, Ahmed Msangi ambaye ameletwa makao makuu ya upelelezi jijini Dar es Salaam.

Msangi amefanywa kuwa mkuu wa kitengo cha makosa dhidi ya binadamu.

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo tarehe 15 Agosti 2018 na msemaji wa jeshi hilo, Kamishena msaidizi wa polisi, Barnabas Mwakalukwa.

“Uhamisho huo ni mabadiliko ya kawaida yanayotokea ndani ya Jeshi la Polisi katika kuongeza ufanisi wa utendaji kazi,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Sehemu ya taarifa hiyo pia imeeleza kuwa  nafasi ya DCP Msangi, imechukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Jonathan Shana.

Naye aliyekuwa mkuu wa operesheni Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Wankyo Nyigesa, amechukua nafasi ya Shana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!