KAMPUNI ya Hyundai East Afrika LTD imezindua magari yake mapya ya kisasa aina ya Tucson toleo la mwaka 2017 katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba), anaandika Hamisi Mguta.
Tucson hiyo mpya ina muonekano mzuri wa kuvutia nje na ndani huku ikiwa imetengenzwa kwa ufanisi wa hali ya juu ambapo kiwango cha uchumi wa mafuta kimeongezwa zaidi ya matoleo ya Hyundai yaliyopita.
“Gari hii mpya ya Tucson imesheheni kile ambacho wateja wetu wanatafuta katika kusaka ushindani wa bei wa kila ngazi, amesema Mehboob Karmali, Mkurugenzi Mtendaji wa Hyundai East Africa LTD.
“Magari ya Hyundai hujulikana kwa mtindo wake safi na mafanikio ya juu, uaminifu wa katika madaraja mbalimbali ya ubora duniani, lengo letu kujitolea kwa bidhaa zetu ni kufanya mambo vizuri. Tunakwenda kuwafurahisha wateja wetu kwa kutoa gari mpya ya kisasa ambayo hawawezi kusahau kwakuwa tunataka kuendelea Kuongoza katika soko na sekta hiyo na kuwafanya wamiliki gari za Hyundai kuwa na faraja,” aliongeza Karmal.
Zaidi ya hayo, Tucson imetengenezwa kwa uendeshaji wa automatic ambayo ina upeo wa usalama wa hali ya juu.
Teknolojia za usalama kama vile breki ya automatiki pindi inapotokea dharura na mfumo wa onyo wa kuondoka.
Mawasiliano ya kiautomatiki ya kuokoa usalama na kamera ya nyuma pia itatolewa.
Hata hivyo kampuni hiyo imetoa gari ya wagonjwa aina ya H-1 ambayo imewekwa kitanda ambacho kina mfumo wa kiautomatiki katika ufungukaji huku visimamio vyake ufunguka vyenyewe.
Antony Nyeupe, Mtendaji mkuu wa mauzo katika Kampuni hiyo amesema gari hiyo ya kubebea wagonjwa ni ya kisasa zaidi na kuwa kampuni hiyo ipo tayari kufanya kazi na mashirika mbalimbali watakayohitaji kununua gari hiyo.
Leave a comment