Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hujuma za uchaguzi zatua bungeni
Habari za Siasa

Hujuma za uchaguzi zatua bungeni

Bunge la Tanzania
Spread the love

HUJUMA zinazofanywa na wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa, zimetua bungeni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Baadhi ya wabunge leo tarehe 5 Novemba 2019, wamelitaka Bunge la Jamhuri kusimamisha shughuli zake na kujielekeza katika kujadili sintofahamu inayoendelea nchini kuhusu zoezi hilo.

Wabunge hao, hususani kutoka vyama vya upinzani, wamemwomba Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika wa Bunge kujadili ukakasi huo, hata hivyo spika hakutoa nafasi.

Maftaha Nachuma, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini amelieleza Bunge, kwamba anashangazwa na wasimamizi wa uchaguzi kupuuza agizo la Suleiman Jafo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI.

Kutokana na malalamiko pia kanuni na taratibu kuvunjwa, Waziri Jafo aliagiza wagombea walioondolewa kwa hila, warejeshwe.

Maftaha amelielekza Bunge, kwamba upinzani una vielelezo mbalimbali kuthibitisha kanuni na taratibu za uchaguzi huo kwenye hatua ya awali ‘zimebakwa’.

Mbunge huyo amemweleza Dk. Tulia, kwamba kama Bunge litaridhia, yupo tayari kukabidhi vielelezo hivyo kwa Job Nduga, Spika wa Bunge.

Anatropia Theonist, mbunge wa Viti Maalum kupitia Chadema, amelalamika hatua ya vyama vya upinzani kufinyangwa nchi nzima.

Amelieleza Bunge kwamba, mambo wanayofanyiwa vyama vya upinzania nchini hayastahili, na kwamba hatua ya Waziri Jafo kutoa kauli ya kutaka walioenguliwa kwa hila, warejeshwe ni kielelezo cha kilio chao.

Frank Mwakajoka, Mbunge wa Tunduma ameonesha hofu yake kutokana na wasimamizi kukiuka kanuni na taratibu kwa makusudi.

Amesema, hatua hiyo inaweza kusababisha sintofahamu nchini ikiwa ni pamoja na machafuko. Ameitaka serikali kuwa makini ili kudumisha amani.

Akijibu hoja hiyo, Dk. Tulia amesema, tayari mamlaka husika zinashughulikia changamoto hiyo kwa kuwa, Waziri Jafo ametoa maelekezo.

Malalamiko ya kuumizwa kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa, tarehe 24 Novemba 2019 yametolewa na vyama mbalimbali vya upinzani.

Miongoni mwa vyama vilivyotoka hadharani na kulalamikia hujuma hizo ni pamoja na Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, Chama cha Umma (Chauma) na Chama cha ACT-Wazalendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!