HOSPITALI moja nchini Uingereza inayofahamika kwa jina la Pinderfields imeingia matatani baada ya kutuhumiwa kutaka kumsabishia mgonjwa Paul Batty (52) kupata maambukizi ya Virusi vya Ukimwi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Batty aliyelazwa hospitalini hapo wiki mbili zilizopita, alilazimika kupima mara kadhaa hospitalini, ili kubaini kama amepatwa na maambukizi ya VVU baada ya kugundua kwamba kitanda alicholalia ndani ya saa 24 wakati alipolazwa hospitalini hapo, kilikuwa na damu ya mgonjwa mwengine.
Batty ambaye ni mkazi wa kijiji cha Fitzwilliam mjini Yorkshire nchini Uingereza alieleza kuwa, anatakiwa kurudi hospitalini miezi mitatu baadae ili apime kama hajapata maambukizi ya VVU na Hepatitis A na B baada ya vipimo vya awali kugundua kwamba hajaathirika.
Akielezea jinsi alivyogundua tukio hilo, Batty aliyeifananisha hospitali hiyo na Jehanam, alisema binti wa rafiki yake aliyemtembelea hospitalini hapo pamoja na mkewe, ndiye aliyeona na kueleza kuhusu uwepo wa damu ya mgonjwa mwengine chini ya kitanda.
Kufuatia tukio hilo, Hospitali ya Mid Yorkshire NHS kwa niaba ya hospitali ya Pinderfields ilimuomba radhi Batty huku ikikiri kuwa, kuna uzembe uliofanywa na baadhi ya watumishi wa hospitali hiyo kwa kutosafisha kitanda hicho kwa wakati.
Leave a comment