Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Hosni Mubarak afariki dunia
Kimataifa

Hosni Mubarak afariki dunia

Hosni Mubarak
Spread the love

RAIS wa zamani wa Mirsi, Hosni Mubarak (91) amefariki dunia leo tarehe 25 Februari 2020, wakati akipatiwa matibabu jijini Cairo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kifo cha Mubarak kimetangazwa leo na Televisheni ya Taifa ya Misri, ambapo imeelezwa kwamba, alifariki dunia katika Hopitali ya Jeshi.

Mtoto wake Alaa amesema, baba yake alikuwa na hali mbaya zaidi Jumamosi iliyopita, na kwamba alifikishwa hospitali na kuwa chini ya uangalizi wa madaktari tangu mwishoni mwa Januari.

Rais Mubaraka aliyeongoza nchi hiyo kwa miaka 30, aliondolewa madarakani kwa maandamano mwaka 2011, kutokana na wananchi kupinga utawala wake kwa kile walichosema kutamalaki kwa umasikini, rushwa na mateso kutoka kwa polisi wake.

Baada ya kuondolewa madarakani, alifikishwa mahakamani na mwaka 2017, alibainika kutenda jinai ya kuua watu wake waliokuwa wakiandamana kumpinga.

Hata hivyo, yapo madai kwamba Mubarak alifariki wiki kadhaa baada ya kufanyiwa upasuaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!