Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu HESLB  yabadili mwongozo wa utoaji mikopo
Elimu

HESLB  yabadili mwongozo wa utoaji mikopo

Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu
Spread the love

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Tanzania (HESLB) imetangaza mwongozo wa utoaji mikopo na ruzuku kwa mwaka wa masomo wa 2019/2020. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 4 Juni 2019 jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru amesema katika mwongozo huo kuna mabadiliko kadhaa ikiwemo kwenye sifa za waombaji, utaratibu wa kuomba mikopo na maelekezo mengine muhimu.

Badru amesema kutangazwa kwa mwongozo huo ni maandalizi ya kukaribisha maombi ya mikopo kwa mwaka ujao wa masomo wa 2019/2020, mchakato unaotarajiwa kuanza tarehe 15 Juni hadi 15 Agosti 2019.

Akitangaza mabadiliko hayo, Badru amesema wanafunzi husika hawatakiwi kuwa na chanzo kingine cha kugharamia masomo yake pamoja na kuwa na vyeti  ikiwemo cha kuzaliwa na cha kifo cha mzazi, vilivyothibitishwa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) au Mamlaka ya Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar.

“Muombaji awe amepata udahili katika chuo kinachofahamika, lazima asiwe na chanzo kingine cha kugharamia masomo yake. Vyeti vya kuzaliwa au cheti cha kifo cha mzazi wake kiwe kimethibitishwa na Wakala wa Usajili wa Matukio ya Kijamii Zanzibar au RITA,” amesema Badru.

Badru amesisitiza kuwa, muombaji atakaye ambatanisha cheti kisichothibitishwa na mamlaka hizo atakosa vigezo vya kupata mkopo.

Amesema lengo la kuweka sharti hilo ni kudhibiti mianya ya udanganyifu kuhusu cheti cha kuzaliwa na cheti cha kifo cha mzazi.

“Kuna mamlaka za kiserikali zimepewa mamlaka ya kuthibitisha cheti cha kuzaliwa, sababu wakati mwingine kinaweza kughushiwa, lazima kila mwanafunzi aambatanishe cheti cha kuzaliwa na kama atakaye ambatanisha ambacho hakijathibitishwa, hicho hakiwezi kutumika wakati wa kutizama maombi yake na vile vile cheti cha kifo,” amesema Badru.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

error: Content is protected !!