Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hatuogopi uchaguzi Singida, tunakataa uharamu – Chadema  
Habari za SiasaTangulizi

Hatuogopi uchaguzi Singida, tunakataa uharamu – Chadema  

Tundu Lissu, mgombea wa Urais wa Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2020 kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema, “kushiriki uchaguzi mdogo katika jimbo la Singida Mashariki, ni sawa na kutenda uovu.” Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Uchaguzi mdogo katika jimbo la Singida Mashariki, lililokuwa likiongozwa na Tundu Lissu, unatarajiwa kufanyika tarehe 31 Julai 2019.

Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC), imetangaza kufanyika uchaguzi huo, kufuatia Spika wa Bunge, Job Ndugai, kutangaza kumvua Lissu ubunge wake, tarehe 28 Juni mwaka huu, wakati wa kuhitimisha mkutano wa Bunge la Bajeti.

Akizungumza na MwanaHALISI ONLINE, leo Jumatatu, tarehe 15 Julai, afisa wa habari wa chama hicho, Tumaini Makene amesema, kwa chama chake, kushiriki uchaguzi huo, ni sawa na kuunga mkono kitendo cha Spika Ndugai kumvua ubunge Lissu.

“Tunakwenda mahakamani, kupigania haki ya wananchi wa Singida Mashariki na wananchi wengine kwa ujumla. Tunakwenda mahakamani kutetea demokrasia na kupinga maamuzi yaliyofanywa na Ndugai na watu wake,” ameeleza Makene.

Alipoulizwa ni lini hasa kesi hiyo itafuguliwa, afisa habari huyo wa Chadema amesema, “mchakato upo kwenye hatua nzuri. Tutawasilisha kesi hii mapema iwezekanavyo ili kuwaondoa wasiwasi wanachama wetu.”

Makene anasema, kumekuwa na muendelezo wa hila katika ubunge wa Lissu hadi kupelekea hata NEC, kuweka muda mchache wa maandalizi ya uchaguzi huo.

“Unaweza kuona hata kwenye ratiba ya NEC wameweka siku 12 za kampeni,” anaeleza na kuhoji, “inawezekanaje kampeni ya kumtafuta mbunge zikafanyika ndani ya siku 12, wakati hata mwenyekiti wa serikali ya mtaa na kitongoji, ni siku 21?”

Wiki iliyopita, NEC ilitangaza kuwa uchaguzi mdogo katika jimbo la Singida Mashariki, utafanyika tarehe 31 Julai 2019, huku ikieleza kuwa ratiba yake inatokana na barua ya Spika Ndugai inayoeleza kuwa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Tundu Antipas Lissu, amepoteza sifa ya kuwa mbunge.

Lissu ambaye ni mmoja wa wanasheria mashuhuri nchini, alitangazwa kuvuliwa ubunge wakati akiwa nje ya nchi kwenye matibabu.

Mwanasiasa huyo, amekuwa nchini Ubelgiji tangu mwanzoni mwa mwaka jana, kufuatia kushambuliwa kwa risasi akiwa nyumbani kwake, eneo la Area D mjini Dodoma, tarehe 7 Septemba 2017.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!