Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hatma ya wabunge nane wa CUF kula kiapo kutolewa leo
Habari za SiasaTangulizi

Hatma ya wabunge nane wa CUF kula kiapo kutolewa leo

Wabunge wa CUF wakizungumza na Wakili wao Peter Kibatala walipokuwa katika Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam leo inatarajiwa kutoa uamuzi wa kuapishwa wabunge wanane walioteuliwa na Profesa Ibrahim Lipumba au wasiapishwe, anaandika Faki Sosi.

Kwa mujibu wa Spika wa Bunge, Job Ndugai, Septemba 5, mwaka huu wabunge wanane walioteuliwa na Lipumba wataapishwa kwa kuwa mpaka sasa ofisi yake haijapokea zuio lolote la mahakama.

Maombi ya kuzuia kuapishwa kwa wabunge wateule yaliwasilishwa Mahakama Kuu na upande unaomuunga mkono, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad.

Maombi hayo yalipingwa na Wakili Mkuu wa Serikali, Gabriel Malata ambaye aliitaka Mahakama kutupilia maombi ya kuzuia wabunge hao wasiapishwe.

Uamuzi huo wa leo mchana utattolewa na Lugano Mwandambo saa nane mchana.
Wabunge waliovuliwa ubunge ni Miza Bakari Haji, Saverina Silvanus Mwijage, Salma Mohamed

Mwassa, Raisa Abdallah Musa na Riziki Shahari Mngwali, Hadija Salum Al- Qassmay, Halima Ali Mohamed na Saumu Heri Sakala wakati madiwani ni Elizabeth Alatanga Magwaja na Layla Hussein Madib.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!