Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Halima Mdee, wanachama wa Chadema wakamatwa jioni hii
Habari za SiasaTangulizi

Halima Mdee, wanachama wa Chadema wakamatwa jioni hii

Spread the love

TAARIFA KWA UMMA

Mwenyekiti wa BAWACHA Taifa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama, Halima Mdee (Mb) pamoja na viongozi wengine, wanachama na wapenzi wa CHADEMA Jimbo la Kawe takriban 13, wamekamatwa na wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kituo cha Polisi Kawe.

Hadi sasa jeshi hilo halijatoa taarifa rasmi kueleza sababu ya kumshikilia mbunge huyo pamoja na wananchi wake baada ya kuwakamata maeneo ya Tanganyika Parkers, Kawe, jijini Dar es Salaam.

Awali, Mdee ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kawe, alisimamishwa na wananchi alipopita maeneo hayo, wakitaka kumpatia kero zao.

Baada ya kusikiliza malalamiko ya wapiga kura wake na kuondoka, inadaiwa polisi walifika eneo hilo na kuanza kuwakamata walioonekana kuwa na sare za CHADEMA.

Alipopata taarifa hizo, Mdee alilazimika kurudi ambapo polisi hao wakiongozwa na Askari Polisi mwenye cheo cha Inspekta walimuamuru Mdee na viongozi hao kuelekea kituoni.

Hadi sasa viongozi hao bado wako kituoni hapo.

Tumaini Makene.

Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano CHADEMA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!