HALIMA Mdee, Mbunge wa Kawe na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake Chadema (BAWACHA), amepokea wito wa Kamanda wa Upelelezi (RCO) Mkoa wa Kipolisi wa Kindoni, kwa ajili ya kufanyiwa mahojiano. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Taarifa ya wito huo imetolewa leo tarehe 23 Februari 2019 na Mdee kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter.
Katika taarifa hiyo, Mdee ameandika kwamba ameitwa kwa ajili ya kuhojiwa katika Kituo cha Polisi cha Oesterbay, huku akieleza kuwa, hajui sababu ya wito huo.
“Nimepata WITO wa KUITWA POLISI OYSTERBAY kwa MAHOJIANO.Mpaka SASA sababu ya wito ni NINI. Ngoja TUJONGEE,” ameandika Mdee katika ukurasa wake wa Twitter.
Nimepata WITO wa KUITWA POLISI OYSTERBAY kwa MAHOJIANO.Mpaka SASA sababu ya wito ni NINI. Ngoja TUJONGEE.
— Halima James Mdee (@halimamdee) February 23, 2019
Leave a comment