MBUNGE wa Kawe, Halima Mdee amefika mbele ya Kamati ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kwa ajili ya kuhojiwa kufuatia kauli za kudhalilisha bunge anazodaiwa kuzitoa mitandaoni. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Mdee amewasili mbele ya kamati hiyo bungeni jijini Dodoma leo tarehe 22 Januari 2019.
Mdee ameingia kwenye kikao hicho kujibu tuhuma zinazomkabili za kumuunga mkono Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad kuhusu kauli aliyoitoa hivi karibuni ya kuliita bunge dhaifu.
Prof. Assad aliitoa kauli hiyo akiwa nje ya nchi wakati akifanyiwa mahojiano na Idhaa ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa (U.N).
Leave a comment