IDADI ya majeruhi wa ajali ya Lori la mafuta ya petrol lililopinduka na kuwaka moto mkoani Morogoro, na kisha kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), inendelea kupungua baada ya wengine wawili kufariki dunia. Anaripoti Bupe Mwakiteleko…(endelea).
Rosijo Mollel (35) alifariki jana mchana tarehe 18 Agosti 2019 ambapo Neema Chakachaka amefariki leo alfajiri tarehe 19 Agosti 2019, wamefanya vifo vilivyotokana na ajali hiyo kufika 97.
Taarifa ya vifo hivyo imetolewa leo na Aminiel Aligaesha, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwenye hospitali hiyo na kwamba, majeruhi waliobaki sasa ni 18.
“Majeruhi hao wanaendelea kupatiwa matibabu ICU (chumba cha uangalizi maalum), amesema Aligaesha
Leave a comment