Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Hakimu, Serikali wakwamisha kesi ya Kabendera
Habari MchanganyikoTangulizi

Hakimu, Serikali wakwamisha kesi ya Kabendera

Mwandishi Erick Kabendera akiwa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
Spread the love

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imehairisha kesi namba 75 ya mwaka 2019 inayomkabili mwandishi wa kujitegemea wa habari za uchunguzi nchini, Erick Kabendera kutokana na upande wa Serikali kushindwa kukamilisha upelelezi. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo Augustina Mmbando, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon ameiomba mahakama hiyo kuahirisha shauri hilo kwa madai kuwa hakimu anayesikiliza shauri hilo Augustine Rwizile amepata dharura pia upande wao haujakamilisha upelelezi wa shauri hilo.

Jebra Kambole ambaye ni Wakili anayeongoza jopo la utetezi ameiomba mahakama hiyo kuwa upande wa Serikali uharakishe upelelezi kutokana na mshtakiwa kuwa hana dhamana.

Nje ya Mahakama hiyo, Mratibu wa Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa amesema kuwa mashtaka yanayomkabili Kabendera yametokana na kazi zake anazozifanya, hivyo wadau wote wa habari na haki za binadamu nchini na ulimwenguni kwa ujumla wanapaswa kupaza sauti zao ili haki itendeke dhidi ya mwandishi huyo.

Aidha Olengurumwa ameviomba vyombo vinavyosimamia utoaji haki nchini ikiwemo vyombo vya uchunguzi kuchunguza kwanza kabla mshtakiwa hajafikishwa mahakamani ili kuepuka wimbi la mrundikano wa kesi nyingi mahakamani kutokana na uchunguzi kutokukamilika.

Kesi hiyo imeahirishwa mpaka Agosti 30, 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watuhumiwa 12 wa kilo 726.2 za dawa za kulevya wafikishwa mahakamani

Spread the love  WATUHUMIWA watatu wamefikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kibaha Mkoani...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari Mchanganyiko

GGML yasisitiza kuendelea kuimarisha afya za wafanyakazi

Spread the loveKAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited kwa kushirikiana na kampuni...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!