MSHAMBULIAJI wa Singida United na timu ya Taifa ya Vijana chini ya umri wa miaka 23, Habib Kyombo amefuzu majaribio ya kucheza soka la kulipwa kwenye klabu ya Mamelodi Sundowns inayoshiriki Ligi Kuu Afrika Kusini. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Mshambuliaji huyo ambae alianza kukipiga kwenye kikosi cha Mbao FC katika msimu wa 2016/17 na kuibuka kuwa mfungaji bora wa kombe la Shirikisho na baadae kutimkia kwenye klabu ya Singida United jana alifanya vipimo vya afya na kufanikiwa kufuzu na kilichobaki ni kumalizana maslahi binafsi.
Septemba 2, 2018 mshambuliaji huyu alipata mwaliko wa kwenda kufanya majaribio ya siku 10 ndani ya klabu hiyo iliyopo kwenye mji wa Pretoria nchini Afrika Kusini na klabu hiyo kufikia maamuzi ya kumsajiri.
Kufanikiwa kwa mshambuliaji huyo kucheza Ligi Kuu Afrika Kusini kutaongeza idadi ya wachezaji raia wa Tanzania ambao wanacheza soka la kulipwa nje ya mipaka ya nchi hii na kuungana na wachezaji kama Simon Msuva, Mbwana Samatta, Himid Mao, Abdi Banda na Hassan Kesi.
Leave a comment