Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Gumzo kutoonekana kwa binti wa Obama
Kimataifa

Gumzo kutoonekana kwa binti wa Obama

Sasha Obama
Spread the love

KUTOONEKANA kwa Sasha Obama, mtoto wa Rais Barack Obama anayemaliza muda wake wa kuliongoza taifa la Marekani katika mkutano wa kuwaaga raia wa nchi hiyo kumeleta minong’ono mingi, anaandika Wolfram Mwalongo.

Sasha mwenye umri wa miaka 15, mtoto wa pili wa Rais Obama hakuonekana ndani ya ukumbi wa McCormick mjini Chicago ambako kiongozi huyo alitoa hotuba kwa mara ya mwisho, akiwa amebakisha siku sita tu kabla ya kuondoka katika Ikulu ya nchi hiyo.

Imekuwa ni kawaida kwa Rais Obama kuambatana na familia yake katika matukio muhimu ya kitaifa, ambapo mkewe Michelle na watoto wake Malia walihudhuria tukio hilo huku Sasha akikosekana na hivyo kuzua maswali.

Hata hivyo, kwa mujibu wa mtandao wa USA Today, inasemekana kuwa Sasha hakuhudhuria mkutano huo kutokana na kukabiliwa na mitihani katika shule ya Sidwell, shule inayotajwa kuongoza kwa kufundisha watoto wa vigogo wa taifa hilo.

Katika hotuba yake ya kuaga Rais Obama alitoa hotuba iliyovuta hisia za wengi huku yeye mwenyewe pamoja na wananchi aliokuwa akiwahutubia wakitokwa machozi mara kadhaa.

Rais Obama alimuelezea mke wake Michelle kama nguzo yake muhimu kwa miaka 25 huku pia akimpongeza kwa namna alivyoifanya Ikulu ya nchi hiyo kuwa mahali pa kila mtu na hata kizazi kipya kumtazama mwanamama huyo kama mtu wa kuigwa.

Rais huyo wa 44 wa Marekani pia aliwaonya raia wa nchi hiyo kutobaguana na kushirikiana katika kuliletea maendeleo taifa hilo katika nyanja mbalimbali ikiwemo uchumi na teknolojia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!