Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Gharika Zimbawe, Msumbiji 120 wafariki
Kimataifa

Gharika Zimbawe, Msumbiji 120 wafariki

Spread the love

ZAIDI ya watu 120 wamepoteza maisha huku kadhaa wakipotea kusikojuliakana kutokana na kimbunga kilichotokea katika nchi ya Msumbiji na Zimbabwe. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kimbunga hicho kinachofahamika kwa jina la Ida, kilianzia nchini Msumbiji usiku wa Alhamisi tarehe 14 Machi 2019 na kusababisha vifo vya watu 62 na baadaye kiliingia nchini Zimbabwe na kuuwa watu 65.

Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa amekatisha ziara yake huku Abu Dhabi kutokana na kimbunga hicho cha Ida.

Waziri wa Mazingira nchini Msumbiji, Celso Correia amesema kimbunga hicho ni janga kubwa kuwahi kushuhudiwa nchini humo.

Mbunge wa Chimanimani nchini Zimbabwe, Joshua Sacco amesema watu kati ya 150 hadi 200 wamepotea kusikojulikana na kwamba vikosi vya ukoaji vinaendelea na shughuli za kuokoa wahanga.

Jana Jumapili wanajeshi walisaidia shughuli za uokoaji na kufanikiwa kuwaokoa wanafunzi 200 walimu na watumishi kadhaa waliokwama katika shule moja iliyoko Chimanimani.

Umoja wa Mataifa nchini Zimbabwe umesema kimbunga cha Ida kimeatihiri watu takribani 10,000.

Hii ni mara ya pili kwa Zimbabwe kukumbwa na janga hilo, ambapo mwezi  Februari mwaka huu watu takribani 40 walifunikwa na vifusi katiika migodi nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!