Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Gambo ajitosa Ubunge Arusha Mjini, Nanai aenda Kawe
Habari za Siasa

Gambo ajitosa Ubunge Arusha Mjini, Nanai aenda Kawe

Spread the love

MRISHO Gambo, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, amechukua fomu kuwania Ubunge Arusha Mjini ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea)

Gambo amechukua fomu leo Jumanne tarehe 14 Julai 2020 kuwania kupitishwa na CCM kuwania ubunge wa Arusha Mjini.

Mbunge anayemaliza muda wake wa jimbo hilo ni Gobdless Lema wa Chadema.

Soma zaidi hapa

Lema; Hata mkiniletea Ccm wote Arusha, nitashinda

Gambo alikuwa mkuu wa mkoa kwa zaidi ya miaka mitatu hadi tarehe 19 Juni 2020 Rais John Pombe Magufuli alipotengua uteuzi wake na kumteua Idd Kimanta.

Soma zaidi hapa 

Rais Magufuli ataja kilichomng’oa Gambo

Gambo alitenguliwa pamoja na viongozi wengine wakiwemo mkuu wa wilaya ya Arusha na Mkurugenzi kwa kile alichoeleza viongozi hao kutokuwa na mahusiano mazuri ya kikazi.

Wakati Gambo akijitoza Arusha Mjini, aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Francis Nanai amechukua fomu kuwania Ubunge wa Kawe jijini Dar es Salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Jimbo hilo limeongozwa kwa miaka kumi mfululizo na Halima Mdee wa Chadema kuanzia 2010-2020

MCL ni wazalishaji wa magazeti ya Mwananchi, MwanaSpoti na The Citizeni.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!