Tuesday , 19 March 2024
Home Gazeti Makala & Uchambuzi Fomu namba 34 A yazua utata uchaguzi Kenya
Makala & UchambuziTangulizi

Fomu namba 34 A yazua utata uchaguzi Kenya

Raila Odinga
Spread the love

MUUUNGANO wa NASA, umetangaza kukataa matokeo huku ukisema matokeo yanayotolewa na Tume ya Uchaguzi ya Kenya, hayana ushahidi wa fomu namba 34 A kama sheria inavyosema, anaandika Irene Emmanuel.

NASA wameomba kukutana na Tume hiyo ili kuangalia ushahidi wa fomu hiyo ya 34 A umefuatwa.

Tamko la NASA limesema kinafanywa sasa na Tume kwa kuacha kuunganisha matokeo na fomu hiyo ambayo ilitakiwa kujazwa na Mawakala na kusainiwa nmi ukiukwaji wa sheria ya uchaguzi.

NASA amesema mpaka sasa fomu hiyo haijaonyeshwa hadharani kwa umma ama wananchi ili wajue matokeo halisi.

Odinga anasema matokeo yote yameathirika kutokana na hiyo fomu kutoonekana.

Kambi ya NASA imeeleza kuwa mengi yamekuwa yakitokea katika uchaguzi huo ikiwemo kuonekana kwa aliyekuwa mtaalamu wa IEBC, Marehemu Chris Musando akiwa bado anaingia katika akaunti ya tume.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CDF Mabeyo: Magufuli alijua anakufa

Spread the love  ALIYEKUWA Mkuu wa Majeshi nchini (CDF), Jenerali Venance Mabeyo,...

AfyaTangulizi

Serikali yafafanua kuondolewa dawa 178 kitita cha NHIF

Spread the loveSERIKALI imesema imeondoa dawa 178 katika kitita cha Mfuko wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ateua, amtumbua Kamishna Ngorongoro

Spread the love  RAIS Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi na utenguzi wa...

Tangulizi

5 mbaroni madai ya Makamba kumng’oa Samia 2025

Spread the loveWATU watano wanashikiliwa na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya...

error: Content is protected !!