FAMILIA ya mfanyabiashara, Mohammed Dewji ‘MO’ na Kampuni za Mohammed Enterprises Tanzania Limited (MeTL) leo wanatarajia kuvunja ukimya juu ya kutekwa kwa bilionea huyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Mkutano huo na waandishi wa habari utafanyika leo tarehe 15 Oktoba, 2018, saa 6.30 mchana katika ofisi za MeTL zilizopo jengo la Golden Jubilee, Posta jijini Dar es Salaam.
Baba wa ‘Mo’ Gullam Dewji amethibitisha uwepo wa mkutano huo na waandishi wa habari wa vyombo vya ndani na nje ya nchi.
Familia ya Dewji inawakaribisha wanahabari kutoka vyombo vyote vya habari katika mkutano utakaofanyika leo saa 6:30 mchana katika ofisi za kampuni ya MeTL Group zilizopo katika jengo la Golden Jubilee Towers ghorofa ya 20 mtaa wa Ohio, Posta jijini Dar es Salaam. pic.twitter.com/ywkFh1KKoe
— MeTL Group (@MeTL_Group) October 15, 2018
Leave a comment