Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko EWURA yatangaza kushusha bei ya Mafuta
Habari Mchanganyiko

EWURA yatangaza kushusha bei ya Mafuta

Spread the love

MAMLAKA ya Udhibiti  wa  Huduma  za  Nishati  na  Maji (EWURA), imetangaza kuwa kuanzia tarehe Mosi Julai, 2017 bei ya mafuta itashuka kwa Sh. 37 kutokana na kushuka  kwa gharama  za usafirishaji  wa  mafuta  katika  soko la dunia, anaandika Yasinta  Francis.

Titus  Kaguo, Meneja  Mawasiliano  na Uhusiano  wa  Ewura amesema  kuwa  bei ya jumla na rejareja  zimepungua  kwa mafuta ya aina zote yani  petroli, dizeli  na mafuta  ya taa.

“Kuanzia Julai mwaka huu, bei za jumla za petroli zinapungua kwa Sh. 37 kwa lita sawa na asilimia 1.92, dizeli shilingi 13.7  kwa lita  sawa na asilimia  0.77  na mafuta ya taa shilingi  18.8 sawa na asilimia 1.10.

“Pamoja  na  ongezeko  la  ushuru   wa  mafuta  ya  petroli  la  shilingi  40  kwa  lita, lakini kuanzia Julai mwaka huu bei za mafuta kwenye soko la ndani  zitapungua kwa kiasi kikubwa,” amesema Kaguo.

Ewura imetangaza kuwa, bei ya mafuta ya petroli kuanzia Julai Mosi, 2017 itakuwa ni Sh. 2,014/- Dizeli Sh. 1,874/- na mafuta ya taa Sh. 1,806/-

“Ewura inawataka wanunuzi wahakikishe wanapata  stakabadhi  ya  malipo  inayoonesha  jina la  kituo, tarehe, aina ya mafuta yaliyonunuliwa na bei  kwa  lita, stakabadhi  hiyo  ya  malipo itatumika kama kidhibiti cha mnunuzi wa mafuta  endapo kutajitokeza malalamiko,” amesema Kaguo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!