Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ester Bulaya atiwa nguvuni Tarime
Habari za Siasa

Ester Bulaya atiwa nguvuni Tarime

Spread the love

ESTER Bulaya, Mbunge wa Bunda Mjini anashikiliwa na polisi wilayani Tarime kwa mahojiano, anaandika Hamisi Mguta.

Imeelezwa kuwa Bulaya amekamatwa kwa kosa la kuhutubia mkutano wa hadhara katika jimbo la Tarime, ambalo si jimbo lake jambo ambalo linakwenda kinyume na agizo la Rais.

Wabunge Esther Matiko na John Heche wameongozana naye kufika katika ofisi ya RCO.

Tumaini Makene, Afisa Habari wa Chadema ameiambia MwanaHALISI Online kuwa Bulaya amekamatwa na yuko kituo cha polisi Tarime Rorya kuhojiwa ni kwanini aliudhuria mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Tarime vijijini uliofanyika jana nyamongo.

“Mikutano ya hadhara inafanyika kwa mujibu wa sheria na sheria haimzuii mtu yoyote kuhudhuria  mikutano ya kisiasa, kama mikutano yetu inaudhuriwa hadi na watu wa CCM, sembuse Ester Bulaya ambaye ni Mjumbe kwenye Kamati Kuu ya chama?,” alihoji Makene.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!