Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Epl yalejea Arsenal, Liverpool, Man City vitani
Michezo

Epl yalejea Arsenal, Liverpool, Man City vitani

Spread the love

BAADA ya kupoteza kwa mchezo kwa mabao 7-2 klabu ya Liverpool kesho watakuwa ugenini kwenye Uwanja wa Goodson Park kujiuliza dhidi ya majirani zao Everton kwenye mchezo wa Ligi Kuu England utakaochezwa majira ya 8 mchana. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Ligi hiyo ambayo ilisimama kwa wiki moja kupisha michezo ya kimashindano na kirafiki ya kimataifa iliyopo kwenye kalenda ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (Fifa) na kesho itashuhudiwa michezo 10 kupigwa kwenye viwanja tofauti.

Katika mchezo huo Liverpool itapata huduma ya wachezaji wao Thiago Alcantara na Sadio Mane ambao walikosekana kwenye mchezo uliopita kutokana kuwa na majeruhi.

Michezo mingine kwenye ligi hiyo itashuhudia Arsenal wataivaa Manchester City kwenye Uwanja wa Etihad, Newcastle United wataialika Manchester United, Chelsea dhidi ya Southampton, Sheffield United kuikabili Fulham na Tottenham dhidi ya West Ham United.

Mpaka sasa Everton wapo juu kwenye msimamo wa Ligi hiyo wakiwa na pointi 12 wakifuatiwa na Astorn Villa kwenye nafasi ya pili wakiwa na pointi 9 sawa na Leicester City, Arsenal na Liverpool.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!