MSHAMBULIAJI wa klabu ya Mbeya City, Eliud Ambokile, amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwezi Septemba wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya kuwashinda wenzake wawili Ibrahim Ajibu wa Yanga na Stamili Mbonde wa Mtibwa Sugar. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).
Ambokile ambaye mpaka sasa ndiyo kinara wa ufungaji kwa wachezaji wa Ligi Kuu baada ya kupachika wavuni mabao sita katika michezo nane aliocheza na klabu yake ya Mbeya City huku akifuatiwa na Meddy Kagere wa Simba mwenye mabao manne.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena mwisho wa juma hili kwa kupigwa michezo kumi kabla ya kwenda mapumziko ili kupisha michezo ya timu za taifa iliyopo kwenye kalenda ya Shirikisho la mpira wa miguu Duniani FIFA.
Leave a comment