Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Elimu ya mkaa endelevu kutolewa kutunza mazingira
Habari Mchanganyiko

Elimu ya mkaa endelevu kutolewa kutunza mazingira

Mkaa endelevu
Spread the love

MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na mazingira, Suleiman Sadiq ameshauri elimu zaidi kutolewa kuhusu Mradi wa Kuleta Mageuzi katika Sekta ya Mkaa nchini (TTCS) maarufu kama mkaa endelevu ili watu wengi wafahamu kwamba mradi huo unasaidia kutunza mazingira na siyo vinginevyo. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Akifungua warsha ya Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero kuhusu tathmini ya mradi huo unaondeshwa katika vijiji katika 11 ndani ya Wilaya hiyo, Sadiq ambaye pia ni Mbunge wa wilaya hiyo alisema, watu wengi bado wakisikia suala la ukataji mkaa wanadhani kila mara ni kuharibu misitu wakati mradi wa TTCS umeonesha kwamba unatunza misitu pia.

Alisema, watu wengi wana elimu ndogo zaidi kuhusu mkaa endelevu ambapo elimu ya kutosha ikitolewa itasaidia kuondoa kupigana na kupishana maelezo juu ya utunzaji wa misitu kwa ujumla kwa kutumia uvunaji misitu wa elimu ya mkaa endelevu.  

Aidha alisema, sheria ya usimamizi wa mazingira ya mwaka 2014 inapaswa kutumika ili kusaidia mradi wa mkaa endelevu kuendelea katika vijiji vya Wilaya ya Mvomero mkoani hapa sambamba na kulinda mazingira kwa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Sadiq pia alishauri mradi huo kutokana na manufaa yake kupanua wigo zaidi katika Wilaya mbalimbali za mkoa wa Morogoro ili nao wapate kunufaika na utunzaji wa mazingira huku wakiboresha kipato kwa kutumia mkaa endelevu.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya hiyo Jonas Zeeland alisisitiza mradi wa TTCS kuendelea kutoa elimu mara kwa mara kwa jamii ili izidi kuufahamu mradi huo wenye kuleta tija tofauti na wanavyofikiria.

Awali Meneja Mradi wa mradi wa TTCS Charles Leonard alisema, Mapato katika wilaya hiyo yamekuwa ni kidogo sana ukilinganisha na wilaya zingine za mradi ikiwemo Morogoro vijijini na Kilosa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya ubovu wa miundombinu ya barabara na ukosefu wa masoko ya uhakika.

Hivyo alisema kwa sasa wanaangalia namna ya kusogeza wateja kwenye vijiji vya mradi huo vilivyopo wilayani humo.

Hata hivyo aliwashauri madiwani wa Halmashauri hiyo kuona namna ya kijipanga kimikakati ili kuweza kuongeza mapato kwenda sambamba na wilaya zingine zenye mradi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!