Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Dudubaya ashikiliwa na Polisi
Habari MchanganyikoMichezo

Dudubaya ashikiliwa na Polisi

Godfrey Tumaini 'Dudubaya'
Spread the love

JESHI la Polisi limeanza kumhoji msanii Godfrey Tumani maarufu kama ‘Dudubaya’ kufuatia tuhuma zinazomkabili za kumdhihaki aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group, Marehemu Ruge Mutahaba. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kamanda wa Polisi Kinondoni, Mussa Taibu leo tarehe 28 Februari 2019 amesema Dudubaya anashikiliwa na polisi kwenye kituo cha Oysterbay jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mahojiano.

Kamanda Taibu amesema Jeshi la Polisi limefungua jalada la uchunguzi wa tuhuma za matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii, na kwamba wakijiridhisha na madai hayo, hatua zaidi za  kisheria zitafuata.

Jeshi la Polisi limechukua hatua hiyo baada ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe jana kuagiza msanii huyo kuchukuliwa hatua kwa kumdhihaki Mrehemu Ruge.

Dudubaya alisambaza katika mitandao ya kijamii video aliyojirekodi akitamka maneno ya kejeli dhidi ya marehemu Ruge, baada ya taarifa za kifo cha Ruge kusambaa.

Ruge alifariki dunia usiku wa tarehe 26 Februari 2019 nchini Afrika Kusini alikokuwa anapatiwa matibabu ya tatizo la figo lililomsumbua kwa zaidi ya miezi minne, ambapo alianza kutibiwa katika Hospitali ya Kairuki iliyoko jijini Dar es Salaam, na baadae akapelekwa India kisha kupelekwa Afrika Kusini ambako umauti ulimfika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!