Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dovutwa ang’olewa UPDP 
Habari za Siasa

Dovutwa ang’olewa UPDP 

Fahmi Dovutwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa UPDP
Spread the love

FAHMI Dovutwa, aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha UPDP, ameondolewa kwenye nafasi hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Imeelezwa, Dovutwa ameng’olewa kwenye nafasi hiyo kwa madai, alikitoa chama hicho katika kushiriki wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, uliofanyika tarehe 24 Novemba 2019.

Kwa mujibu wa Abdalla Mohammed Khamis, Kaimu Mwenyekiti wa UPDP,  Dovutwa amevuliwa uenyekiti na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho.

Khamis amesema Dovutwa amepewa adhabu hiyo kufuatia hatua yake ya kutangaza UPDP hakitashiriki uchaguzi huo, pasina kupewa ridhaa na uongozi wa chama hicho.

Ameeleza kuwa, kitendo hicho ni kinyume na katiba ya UPDP, pia, kimesababisha chama hicho kukosa wenyeviti wa serikali za mitaa.

Uchaguzi wa serikali za mitaa ulifanyika pasina ushiriki wa vyama vya upinzani nane, ikiwemo chama cha UPDP.

Vyama hivyo, vilisusa kushiriki uchaguzi huo kwa madai kuwa, mchakato wake ulikiuka kanuni za uchaguzi huo.

 

 

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari za Siasa

Rais Samia ampongeza mpinzani aliyeshinda urais Senegal

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amempongeza mwanasiasa wa...

Habari za Siasa

Ushindi wa mpinzani Senegal wakoleza moto kwa wapinzani Tanzania

Spread the loveUSHINDI wa aliyekuwa mgombea  urais wa upinzani nchini Senegal, Bassirou...

error: Content is protected !!