Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Dodoma wasaka mwarobaini ufaulu wa wanafunzi
Elimu

Dodoma wasaka mwarobaini ufaulu wa wanafunzi

Dk. Binirith Mahenge, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Spread the love

KASIM Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anatarajiwa kuwa ngeni rasmi katika uzinduzi wa Kongamano la Elimu Mkoa wa Dodoma. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kwa mujibu wa Dk. Binirith Mahenge, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, kongamano hilo litafanyika tarehe 21 – 22 Machi 2020, katika ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Mipango jijini humo.

Dk. Mahenge amesema, kongamano hilo litahusisha wadau wa elimu, kwa lengo la kujadili juu ya kushuka kwa elimu katika mkoa wa Dodoma, sambamba na kutafuta njia ya kuiboresha elimu.

Amesema, kongamano hilo litajielekeza zaidi kujua ni kwanini wanafunzi wamekuwa wakifanya vibaya shuleni, pia kujadili mambo mbalimbali ambayo yanaweza kuwa changamoto kwa wanafunzi wa mkoa huo.

“Msukumo wa kuandaa kongamano hili umetokana na ukweli, kuwa hali ya maendeleoya elimu siyo nzuri na ufaulu kimkoa siyo wa kudhisha. Vipo baadhi ya viashiria ambavyo tumevibaini tukaona vinapelekea kushuka kwa kiwancha elimu mkoani,” amesema Dk. Mahenge.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!