Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Vincent Mashinji azomewa kortini
Habari za Siasa

Dk. Vincent Mashinji azomewa kortini

Spread the love

DAKTARI Vincent Mashinji, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kabla ya kujiunga Chama cha Mapinduzi (CCM), amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuzomewa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Leo tarehe 10 Machi 2020, Dk. Mashinji alikutana na zogo wakati anaingia katika chumba cha mahakama hiyo, kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya Kesi ya Uchochezi Na.112/2018, inayomkabili na viongozi wakuu wa Chadema.

Alipokuwa anaingia katika chumba cha mahakama hiyo, Dk. Mashinji alianza kuzomewa na baadhi ya wafuasi wa Chadema.

Hata hivyo, alivyoingia Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema, shangwe ziliibuka huku watu wakiimba ‘Mwamba tuvushe’.

Muda huu watu wanaanza kuingia katika chumba cha mahakama kwa ajili ya kusubiri hukumu ya viongozi hao.

Washtakiwa katika kesi hiyo ni pamoja na Halima Mdee, Mwenyekiti Bawacha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!