Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Tulia amdhibiti Mbunge wa CCM
Habari za Siasa

Dk. Tulia amdhibiti Mbunge wa CCM

Dk. Tulia Ackson, Naibu Spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

TULIA Ackson, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemtaka Rashidi Shangazi, Mbunge wa Mlalo, mkoani Tanga kufuta kauli yake juu ya Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, baada ya kuiita kambi hiyo kuwa ni kambi rasmi ya upotoshaji, anaandika Hellen Sisya.

Tukio hilo limetokea leo bungeni mjini Dodoma katika kikao cha mwisho cha bunge ambapo mbunge huyo alikuwa akichangia mjadala unaohusu miswada mitatu ya ulinzi wa rasilimali na maliasili za nchi.

Kauli ya Mbunge huyo ilimnyanyua kitini Abdallah Mtolea, Mbunge wa Temeke (CUF) ambaye aliomba utaratibu kwa mujibu wa kanuni za bunge akitaka Shangazi afute maneno yake kwani ni kinyume cha kanuni hizo.

Naibu Spika alikubaliana na hoja ya Mtolea na kumtaka mbunge huyo kuheshimu kanuni za bunge na kuondoa maneno ya kuudhi aliyoyasema na badala yake kutumia maneno sahihi yanayotakiwa.

“Mheshimiwa Rashid Shangazi, naomba ufute maneno uliyoyasema kwasababu ni kinyume cha kanuni za bunge. Weka maneno yanayotakiwa kuwepo,” alisema Dk. Tulia.

Agizo hilo lilitekelezwa na Mbunge huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!