Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Tulia akwepa ofisi ya Sugu
Habari za Siasa

Dk. Tulia akwepa ofisi ya Sugu

Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Dk. Ackson Tulia ameamua kutumia sehemu ya jengo la Mkuu wa Wilaya ya Mbeya kufanya majukumu yake ya kibunge badala ya ofisi ya mbunge. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya…(endelea).

Akieleza sababu za kukwepa ofisi iliyokuwa ikitumiwa na Joseph Mbilinyi maarufu Sugu (Chadema), aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Dk. Tulia amesema ‘nimekwepa mlolongo wa kukabidhiana ofisi.’

“Ningesema nisubiri makabidhiano ya ofisi, nitavuta muda mwingi kama mnavyojua,” amesema Dk. Tulia muda mfupi baada ya kukutana na wananchi na kusikiliza kero zao.

Dk. Tulia Ackson

Dk.  Tulia ambaye ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri, alitangazwa kumshinda Sugu, hata hivyo ushindi wake umeingia ukakasi baada ya Sugu na vyama vya upinzani nchini kukosoa mchakato mzima wa uchaguzi mkuu kwamba, uligubikwa na hila.

Miongoni mwa vipaumbele vya Dk. Tulia kwa wakazi wa jimbo lake ni pamoja na kujenga kiwanda cha taulo za kike, kuimarisha huduma za za afya, kuboresha miundombinu ya elimu, kuboresha soko la wafanyabishara wadogo kwenye eneo la uwanja wa ndege wa zamani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!