Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Askofu Shoo agonja kisu kwenye mfupa
Habari za SiasaTangulizi

Askofu Shoo agonja kisu kwenye mfupa

Askofu Mkuu wa KKKT Askofu Dk. Frederick Shoo
Spread the love

TABIA ya utekaji, utesaji, unyongaji haki, dhuluma na kiburi inayolalamikiwa nchini, imekemewa vikali na Dk. Frederick Shoo, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT). Anaripoti Mwandishi Wetu, Moshi … (endelea).

Akitoa salamu za Krismasi kwenye ibada iliyofanyika katika Kanisa la KKKT, Usharika wa Moshi Mjini mkoani Kilimanjaro leo tarehe 25 Desemba 2019, Dk. Shoo amewataka watu waliojaa viburi vinavyojengwa na nafasi zao za uongozi, waache ili wawe salama mbele ya Mungu.

Kiongozi huyo wa dini amesema, watu waliompokea Yesu mioyo yao haina kiburi  wala majivuno. Amesema, kuna watu wanaotesa wenzao wasiokuwa na hatia jambo ambalo halimfurahishi Mungu.

“Yesu Kristo akatuguse mioyo yetu, tubadilike, tuache kiburi, tuache kuwatesa binadamu wenzetu na tuache kufurahia kuwatesa wenzetu wasio na hatia,” amesema Dk. Shoo.

Licha wateswaji kukumbana na matuio ya kikatili kutoka kwa wenye mamlaka, Dk. Shoo amewatia moyo kwamba, mateso yao hayapotei na kwamba ipo siku mateso ya watesaji yatafika ukomo wake.

“Katika kuteseka kwenu, kwa namna yoyote ile, hata tunapoteswa bila hatia, tujue kwamba Mungu yupo pamoja nasi, hivyo usiogope na usikate tamaa wala kuondoa tumaini lako kwa Mungu,  kwani mateso unayokutana nayo kwenye maisha, jua hakika yana mwisho wake,” amesema Dk. Shoo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!