Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Shika aendelea kusota, Polisi kumpima akili
Habari Mchanganyiko

Dk. Shika aendelea kusota, Polisi kumpima akili

Spread the love

KAIMU Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika amesema jeshi la polisi linaendelea kummshikilia Dk. Louis Shika kwa kuwa bado linaendelea na uchunguzi huku wakijipanga kumfanyia vipimo vya akili, anaandika Angel Willium.

Kitalika amesema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani muda wowote baada ya uchunguzi kukamilika, lakini hadi sasa hakuna ndugu yake yeyote aliyejitokeza kushirikiana na jeshi la polisi katika uchunguzi unaoendelea.

Kamanda amesema kabla ya kumfikisha mahakamani jeshi la polisi linawasiliana na mamlaka nyingine za serikali kuangalia kama kuna uwezekano wa kumpima Dk. Shika kama ana matatizo ya akili.

Dk Shika anatuhumiwa kwa kuvuruga mnada wa nyumba za bilionea Said Lugumi ulioendeshwa na kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart baada ya kushindwa kulipa asilimia 25 ya malipo ya awali ya gharama za nyumba hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!