Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Shika aendelea kusota, Polisi kumpima akili
Habari Mchanganyiko

Dk. Shika aendelea kusota, Polisi kumpima akili

Spread the love

KAIMU Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Benedict Kitalika amesema jeshi la polisi linaendelea kummshikilia Dk. Louis Shika kwa kuwa bado linaendelea na uchunguzi huku wakijipanga kumfanyia vipimo vya akili, anaandika Angel Willium.

Kitalika amesema mtuhumiwa huyo atafikishwa mahakamani muda wowote baada ya uchunguzi kukamilika, lakini hadi sasa hakuna ndugu yake yeyote aliyejitokeza kushirikiana na jeshi la polisi katika uchunguzi unaoendelea.

Kamanda amesema kabla ya kumfikisha mahakamani jeshi la polisi linawasiliana na mamlaka nyingine za serikali kuangalia kama kuna uwezekano wa kumpima Dk. Shika kama ana matatizo ya akili.

Dk Shika anatuhumiwa kwa kuvuruga mnada wa nyumba za bilionea Said Lugumi ulioendeshwa na kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart baada ya kushindwa kulipa asilimia 25 ya malipo ya awali ya gharama za nyumba hizo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!