Tuesday , 16 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Shein: Tujifunze utawala bora kwa Mkapa
Habari za Siasa

Dk. Shein: Tujifunze utawala bora kwa Mkapa

Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Dk. Ali Shein, Rais wa Zanzibar amewataka viongozi wa sasa kujifunza utawala bora kutoka kwa Hayati Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam …. (endelea).

Amesema, Mzee Mkapa aliyefariki usiku wa kuamkia jana tarehe 24 Julai 2020, jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa tayari ameacha funzo la utawala bora kwa viongozi wa sasa na wajao.

Dk. Shein ametoa kauli hiyo leo tarehe 25 Julai 2020, nyumbani kwa Mkapa, Masaki jijini Dar es Salaam, alipokwenda kuipa pole familia ya rais huyo.

Amesema, viongozi waliopo madarakani wanapaswa kujifunza kutokana na uongozi wa Rais Mkapa, aliyeongoza Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005.

“Viongozi waliopo madarakani wanapaswa wajifunze kwa marehemu Mkapa, wajifunze uongozi wake. Wale viongozi wa leo tujifunze na amesadifu vizuri. Ameandika kitabu chake,” amesema Rais Shein na kuongeza:

“Tumepata msiba mkubwa kwenye taifa letu na kwa Afrika. Mkapa ni kiongozi wetu, sisi wengine ametulea. Mimi aliniteua Makamu wa Rais, nilifanya naye kazi karibu miaka minne na nusu na nimejifunza mengi,” amesema.

Dk. Sheikn amesema, Mzee Mkapa aliitumikia nchi kwa heshima na nidhamu kubwa, alisimamia misingi ya uchumi wa nchi na maendeleo yake.

Amesema, atamkumba Rais Mkapa kwa mambo mengi ikiwemo uanzishwaji wa utawala bora pamoja na kuleta mageuzi ya kiuchumi.

“Nayakumbuka mengi sana, amesaidia kuibadilisha nchi. Ameanzisha utawala bora, amebadilisha uchumi na alikua wa kwanza kuanzisha Wizara ya Utawala Bora Afrika,” Amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

Habari za Siasa

Nape: Wanasiasa, wanahabari, wafanyabiashara mteteeni Samia

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,...

Habari za Siasa

CAG: TAWA imegawa vibali vya uwindaji bila idhini ya waziri

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!