Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Dk. Ndugulile atembelea MOI, akagua chumba cha tiba mtandao
Afya

Dk. Ndugulile atembelea MOI, akagua chumba cha tiba mtandao

Dk. Faustine Ndungulile, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (katikati) akikagua wodi ya kutibu kwa mtandao
Spread the love

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile ametembelea Taasisi ya Tiba ya mifupa, upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu (MOI) kukagua maendeleo ya chumba maalum cha Tiba mtandao ambacho kinatarajia kukamilika na kufanya kazi kuanzia mwezi Juni mwaka huu. Anaripoti Hamisi Mguta … (endelea).

Awali akiwa kwenye taasisi hiyo ya MOI, Dk. Ndugulile aliweza kupokea maendeleo ya ukamilishwaji wa chumba hicho cha tiba mtandao ambapo pia aliwataka kuhakikisha wanasimamia vizuri uendeshaji wake kwani utasaidia Taifa kutoa huduma za kibingwa sehemu kubwa zaidi hapa nchini zikiwemo hospitali za rufaa za mikoa na nyingine 

Aidha, Dk. Ndugulile amewataka kukamilisha hatua zote za chumba hicho na kitakapokamilika uzinduzi ufanyike kama inavyotarajiwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Dk. Respicious Boniface amesema kuwa, chumba hicho kinategemea kukamilika na kuanza kufanya kazi mwezi Juni mwaka huu na kitakapokamilika kitasaidia matibabu kwa kwa njia ya mtandao nchi nzima.

“Chumba cha Tiba mtandao hapa MOI kitakapokamilika hospitali zote kubwa za rufaa za mikoa na zingine za Rufaa, zitatuma picha hapa na watalaam wa MOI wanatoa majibu na kurudisha tiba kule na kutoa ushauri wa jinsi wa kutoa matibabu kwa wagonjwa wakiwa hukohuko,” alieleza Dk. Boniface.

Chumba hicho cha tiba mtandao kinatarajiwa kuwepo kwenye jengo jipya la MOI ambapo tayari timu ya watalaam wanaendelea na taratibu za kukamilisha uendeshaji wake.

MOI ni miongoni mwa Taasisi za tiba zenye kutoa huduma za kibingwa huku ikiwa na Madaktari wabobezi kwenye tiba ya mifupa, upasuaji wa ubongo, mgongo na mishipa ya fahamu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!