Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwinyi, Maalim Seif ni ‘kazi kazi’ Z’bar
Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mwinyi, Maalim Seif ni ‘kazi kazi’ Z’bar

Spread the love

KAZI ya kumwaga sumu ya ubaguzi miongoni mwa Wazanzibari, inayofanywa na Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na makamu wake wa kwanza Maalim Seif Sharif Hamad, sasa inashika kasi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Pemba…(endelea).

Wakati Dk. Mwinyi akiwaambia wakazi wa Pemba kwamba, lengo la Serikali ya Umoja wa Kitaifa (SUK), visiwani humo ni kuimarisha amani, Maalim Seif amewaambia wakazi hao kuwa suala la amani sio la hiyari.

Dk. Mwinyi na Maalim Seif wametoa kauli hiyo wakati walipozungumza kwenye mkutano wa mkuu wa pili wa amani uliofanyika Unguja tarehe 16 Januari 2021.

Dk. Mwinyi ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar amesema, anachokitaka kwenye serikali yake ni kudumisha na kuimarisha amani, umoja na mshikamano kwa Wazanzibari wote.

Dk. Mwinyi amewaambia wajumbe wa mkuano huo kwamba, Katiba ya Zanzibar yam waka 1984, imetoa kipaumbele kikubwa katika suala la amani.

Na kwamba, atafanya awezalo kuhakikisha malengo ya waasisi wa taifa hilo kuhusu amani, umoja na mshikamano yanafikiwa kwa manufaa ya ustawi wa viziwa hivyo viwili.

Wakati huo, Maalim Seif ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, amesema maridhiano hayo yanapaswa kulelea na kuwa na tija ili vizazi vijavyo viweze kusoma historia na kurithi.

Chama cha ACT-Wazalendo mwishoni mwa mwaka jana, kiliridhia kujumuika katika kuunda SUK, licha kushutumu chama tawala -Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kuvuruga uchaguzi uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2021.

Awali, ACT-Wazalendo kiligoma kushiriki kwenye serikali hiyo licha ya kupata zaidi ya silimia 10 ya kura iliyohitajika na Katiba ya Zanzibar ili kuingia kwenye muundo wa seikali.

Mabalozi wa Nchi za Ulaya waliohudhuria mkutano huo, wameeleza kuwa na matumaini makubwa ya Zanzibar kupiga hatua kutokana na hatua za awali kuchukuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!