Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwinyi kuingia Ikulu leo
Habari za Siasa

Dk. Mwinyi kuingia Ikulu leo

Spread the love

DAKTARI Hussein Ali Mwinyi, leo Jumatatu tarehe 2 Novemba 2020 ataapishwa kuwa Rais wa nane wa Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea)

Shughuli hiyo ya uapisho, itafanyika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid ambapo Dk. Mwinyi mwenye miaka 53 anachukua nafasi inayoachwa wazi na Rais Ali Mohamed Shein.

Rais Shein, anamaliza ungwe yake ya miaka kumi ya utawala kwa mujibu wa Katiba aliyoianza tarehe 3 Novemba 2010.

Dk. Mwinyi ambaye ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, anaapishwa baada ya kutangazwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) kuibuka mshindi wa Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 27 na 28 Oktoba 2020.

          Soma zaidi:-

Dk. Mwinyi alitangazwa tarehe 29 Oktoba 2020 na Mwenyekiti wa ZEC, Jaji Hamid Mahmoud Hamid kwa kupata kura 380,402 sawa na asilimia 76.27 ya kura zote 382,402.

Jaji Hamid alisema, Maalim Seif Sharif Hamad wa ACT-Wazalendo alipata kura  99,103 sawa na asilimia 19.87.

Dk. Mwinyi atakuwa Rais wa nane wa visiwa hivyo tangu kufanyika kwa Mapinduzi ya Zanzibar tarehe 12 Januari 1964.

Dk. Mwinyi aliyezaliwa tarehe 23 Desemba 1966 ni mtoto wa Ali Hassan Mwinyi, aliyekuwa Rais wa Zanzibar kwa siku 267 kisha Rais wa Tanzania kati ya mwaka 1985 hadi 1995.

Marais wengine walimtangulia na miaka yao kwenye mabano wa kwanza ni;  Abeid Karume (26 Aprili 1964- 7 Aprili 1972), Aboud Jumbe (7 Aprili 1972- 30 Januari 1984), Ali Hassan Mwinyi (30 Januari 1984- 24 Oktoba 1984), Idris Abdul Wakil (24 Oktoba 1985- 25 Oktoba 1990).

Salmin Amour (25 Oktoba 1990- 8 Novemba 2000), Aman Abeid Karume (8 Novemba 2000- 3 Novemba 2010) na Dk. Ali Mamohed Shein aliingia 3 Novemba 2010 hadi leo Jumatatu anapokabidhi madaraka kwa Dk. Mwinyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!