Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mwinyi arejesha fomu, asifu demokrasia CCM
Habari za Siasa

Dk. Mwinyi arejesha fomu, asifu demokrasia CCM

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk. Hussein Mwinyi akirejesha fomu za kuwania Urais wa Zanzibar ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Spread the love

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk. Hussein Mwinyi amerejesha fomu za kuwania Urais wa Zanzibar ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Dk. Mwinyi ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi alikuwa wa tano kati ya wagombea 26 kuchukua fomu hizo katika Ofisi Kuu za CCM, zilizopo Ugunja visiwani humo tarehe 17 Juni 2020.

Baada ya kukabidhiwa fomu hizo, Dk. Mwinyi alisema asingeweza kuongea lolote na anachofanya, anakwenda kuzipitia fomu hizo na kuona kuna nini anapaswa kukifanya. Kubwa ni kutafuta wadhamini wasiopungua 250.

Leo Jumatano mchana tarehe 24 Juni 2020, Dk. Mwinyi amerejesha fomu hizo huku akizungumza kwa ufupi kuwa, “chama chetu kina demokrasia ya hali ya juu, kila aliyetaka anaruhusiwa.”

Dk. Mwinyi ambaye pia ni Mbunge wa  Kwahani amesema kwa sasa anaacha  mchakato wa ndani wa chama kuendelea.

Wagombea waliochukua fomu ni;

  1. Mbwana Bakari Juma
  2. Ali Abeid Karume
  3. Mbwana Yahya Mwinyi :
  4. Omar Sheha Mussa
  5. Hussein Ali Mwinyi
  6. Shamsi Vuai Nahodha
  7. Mohammed Jaffar Jumanne
  8. Mohammed Hijja Mohammed
  9. Issa Suleiman Nassor
  10. Makame Mnyaa Mabarawa
  11. Mwatum Mussa Sultan
  12. Haji Rashid Pandu
  13. Abdulhalim Mohammed Ali
  14. Jecha Salum Jecha
  15. Dk Khalid Salum Mohammed
  16. Rashid Ali Juma
  17. Khamis Mussa Omar
  18. Mmanga Mjengo Mjawiri
  19. Hamad Yussuf Masauni
  20. Mohammed Aboud Mohammed
  21. Bakari  Rashid Bakari
  22. Hussein Ibrahim Makungu
  23. Ayoub Mohammed Mahmoud
  24. Hashim Salum Hashim
  25. Hasna Atai Masound
  26. Fatma Kombo Masound

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!