WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk. Hussein Mwinyi amerejesha fomu za kuwania Urais wa Zanzibar ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).
Dk. Mwinyi ambaye ni mtoto wa Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi alikuwa wa tano kati ya wagombea 26 kuchukua fomu hizo katika Ofisi Kuu za CCM, zilizopo Ugunja visiwani humo tarehe 17 Juni 2020.
Baada ya kukabidhiwa fomu hizo, Dk. Mwinyi alisema asingeweza kuongea lolote na anachofanya, anakwenda kuzipitia fomu hizo na kuona kuna nini anapaswa kukifanya. Kubwa ni kutafuta wadhamini wasiopungua 250.
Leo Jumatano mchana tarehe 24 Juni 2020, Dk. Mwinyi amerejesha fomu hizo huku akizungumza kwa ufupi kuwa, “chama chetu kina demokrasia ya hali ya juu, kila aliyetaka anaruhusiwa.”
Dk. Mwinyi ambaye pia ni Mbunge wa Kwahani amesema kwa sasa anaacha mchakato wa ndani wa chama kuendelea.
Wagombea waliochukua fomu ni;
- Mbwana Bakari Juma
- Ali Abeid Karume
- Mbwana Yahya Mwinyi :
- Omar Sheha Mussa
- Hussein Ali Mwinyi
- Shamsi Vuai Nahodha
- Mohammed Jaffar Jumanne
- Mohammed Hijja Mohammed
- Issa Suleiman Nassor
- Makame Mnyaa Mabarawa
- Mwatum Mussa Sultan
- Haji Rashid Pandu
- Abdulhalim Mohammed Ali
- Jecha Salum Jecha
- Dk Khalid Salum Mohammed
- Rashid Ali Juma
- Khamis Mussa Omar
- Mmanga Mjengo Mjawiri
- Hamad Yussuf Masauni
- Mohammed Aboud Mohammed
- Bakari Rashid Bakari
- Hussein Ibrahim Makungu
- Ayoub Mohammed Mahmoud
- Hashim Salum Hashim
- Hasna Atai Masound
- Fatma Kombo Masound
Leave a comment