Tuesday , 19 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Dk. Mwakyembe atonesha vidonda vya Azory
Habari Mchanganyiko

Dk. Mwakyembe atonesha vidonda vya Azory

Spread the love

WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, amepuuza kilicho cha muda mrefu cha wadau wa habari nchini cha kutaka kuelezwa mahali aliko, mwandishi wa gazeti la Mwananchi, Azory Gwanda. Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni leo Jumanne, Dk. Mwakyembe, ametaka kupuuzwa kwa watu wanaotaka ripoti kamili ya kupotea kwa Azory. Alikuwa ahitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha ujao wa fedha.

Mteule huyo wa Rais John Magufuli, amedai kushangazwa kwake na wanaofuatilia mahali aliko Gwanda, na kuongeza, “kama kupotea, waliopotea wako wengi.”

Azory Gwanda ametoweka katika mazingira ya kutatanisha tokea tarehe 21 Novemba 2017. Mpaka sasa, hakua ripoti yoyote iliyotolewa kutoka chombo chochote cha ulinzi na usalama juu ya kupotea kwake.

Mke wake, Anna Pinoni, alinukuliwa akisema, “…watu wapatao wanne, wakiwa kwenye gari aina ya Toyota Land Cruiser, yenye rangi nyeupe, walimchukua mume wake (Azory Gwanda), kutoka katikati ya mji huo, mahali ambapo hupendelea kukaa.

“Kwamba, aliporudi nyumbani alikuta vitu vimezagaa, ishara kuwa waliipekua nyumba yao.”

Mwandishi huyo mahiri wa habari, alikuwa akiishi na kufanyia shughuli zake katika mji mdogo wa Kibiti, mkoani Pwani.

Alikuwa mmoja wa waaandishi wa kwanza kabisa wa habari, kuripoti kwa kina, juu ya mfululizo wa mauwaji, yaliyokuwa yakitekelezwa katika eneo hilo.

Akitetea hoja yake ya kutaka wananchi kipuuza taarifa za kumtafuta mwandishi huyo, Dk. Mwakyembe amesema, kuna watu wengi wamepotea katika eneo hilo, wakiwemo vongozi wa serikali.

Ameapa kuwa “serikali itaendelea kuwadhibiti watu wanaokiuka utoaji wa maoni, kwa kuwa hakuna uhuru usiokuwa na mipaka.” Hakufafanua.

Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wa kisiasa, wanaitafsri kauli yake kuwa yawezekana kwa kuwa serikali ina mikono mirefu, inafahamu ya kupotea kwa mwandishi huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Diwani, wananchi wengine 463 wahama Ngorongoro

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro ambaye pia...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Shule zafungwa kutokana na ongezeko la joto

Spread the loveSUDAN Kusini imeamuru kufungwa kwa shule zote kuanzia leo Jumatatu,...

Habari Mchanganyiko

Bunge laja na Marathon kuchangia ujenzi wa sekondari

Spread the loveBUNGE la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania linatarajia kukusanya fedha...

error: Content is protected !!