Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Mpango: Tusisalimu amri
Habari za Siasa

Dk. Mpango: Tusisalimu amri

Dk. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

DAKTARI Phillip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango amezitaka nchi za Afrika kutosalimu amri, kwa mataifa ya kigeni, yanayohatarisha uhuru wa kujitawala. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Dk. Mpango ametoa kauli hiyo jana tarehe 25 Oktoba 2019, katika Kongamano Maalumu la Vita vya Kiuchumi na Hatma ya Afrika, lililofanyika jijini Dar es Salaam.

“Kamwe tusisalimu amri, kwa wale wanaojaribu kupinda mikono yetu na kuhatarisha uhuru wetu wa kujitawala,” amesema Dk. Mpango.

Waziri huyo wa fedha ameeleza kuwa, nchi za Afrika zimepata uhuru wa kisiasa lakini zimekosa uhuru wa kiuchumi.

“Tumepata uhuru wa kisiasa, lakini uhuru wa kiuchumi bado. Fikra za utegemezi, uhisani bado zipo. Inabidi tuzipige vita. Lakini pili, Afrika lazima izingatie misingi ya usimamizi wa uchumi. Ni lazima nchi zetu tuzielekeze kupanua wigo wa kiuchumi kwa upande wa uzalishaji masoko na mtaji,” amesema Dk. Mpango.

Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amesema nchi za Afrika zilizoamua kujitegemea ziko vitani kutokana na vitimbi vya mataifa yaliyoendelea.

“Tuko vitani, tunaishi kwenye nchi za vitimbi hasa kwa mataifa yanayoamua kujitegemea,” amesema Prof. Kabudi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!