Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Magufuli: Sikustahili urais
Habari za Siasa

Dk. Magufuli: Sikustahili urais

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amesema kuwa, hakustahili kuwa Rais wa Tanzania bali Watanzania wenyewe ndio waliomchagua. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Amesema, wananchi wa Mbarali mkoani Mbeya na maeneo mengine ya nchi, ndio walimuona anafaa kushika wadhida huo kati ya wale waliokuwa wanagombea.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo tarehe 2 Aprili 2019, wakati akituhutubia mkutano wa hadhara mjini Mabarali akiwa kwenye mwendelezo wake wa ziara ya siku nane.

Akihutubia kwenye mkutano huo, Rais Magufuli amesema hakustahili kuwa rais, bali wananchi wa Tanzania walikuwa na sababu za msingi za kumchagua.

Na kwamba, Watanzania waliamua kumchagua kwa kuwa, waliamini anaweza kutatua matatizo yao hasa ya wanyonge.

“Mlinichagua kuwa kiongozi wenu, sikustahili kuwa Rais, mliamua kuwa Magufuli tunampa urais. Sasa tuna miaka mitatu kwenye uongozi na tuliahidi kutekeleza Ilani ya CCM, mawaziri wameeleza tuliyofanya na ambayo bado hayajafanyika wameeleza changamoto zake,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!