Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Magufuli kuapishwa kesho, mataifa 17 kuhudhulia
Habari za Siasa

Dk. Magufuli kuapishwa kesho, mataifa 17 kuhudhulia

Rais John Magufuli
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imesema, viongozi wa ngazi za juu na wawakilishi wa nchi zaidi ya 17 wamethibitisha kuhudhulia sherehe ya kumwapisha Dk. John Pombe Magufuli kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kesho Alhamisi tarehe 5 Novemba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Dk. Magufuli ataapishwa katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma ili kuhitimisha muhula wa pili na wa mwisho wa miaka mitano kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania inayoeleza Rais atakaa madarakani kwa miaka kumi.

Rais huyo mteule kupitia Chama tawala-CCM, alitangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania (NEC) kuwa mshindi kwa kupata kura milioni 12 sawa na asilimia 84 ya kura zilizopigwa milioni 15 huku mshindani wake, Tundu Lissu wa Chadema akipata kura milioni 1.9 sawa na asilimia 13 ya kura zote.

Leo Jumatano tarehe 4 Novemba 2020, Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Dk. Hassan Abbas akizungumza akiwa Uwanja wa Jamhuri Dodoma kunakofanyika maandalizi ya mwisho ya sherehe hizo, amesema wageni mbalimbali wamethibitisha kuhudhulia.

Dk. Abbas amesema, ni kwa mara ya kwanza sherehe za kuapishwa kwa Rais wa Tanzania zinafanyikia Dodoma makao makuu ya nchi jambo ambalo ni historia inayoendana na kumuenzi Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Amesema, viongozi wa juu na wawakilishi kutoka zaidi ya mataifa 17 wamethibitisha kuhudhulia sherehe hizo zitakazoanza asubuhi.

Amewataja baadhi ya viongozi hao ni marais, Yoweri Mseveni (Uganda), Emmerson Mnangagwa (Zimbabwe), Azali Assoumani (Comoro) na Rais mstaafu wa Nageria, Olusegun Obasanjo.

Dk. Abbas ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amesema, Mhubiri mashuhuri raia wa Nigeria, TB Joshua naye atakuwepo, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Mabalozi,

Msemaji huyo wa Serikali amesema, kutokana na ushindi alioupata Dk. Magufuli, salamu kutoka mataifa zadi ya 32 zimetolewa na zinaendelea kutolewa.

1 Comment

  • Congratulations to you Hon. J P.Magufuli. We hope you will be more generous n responsible enough to fulfill all what you have promised during your campaigns.
    God bless you.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!