Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Lwaitama: Ni uhuru wa mawazo wa wabunge Chadema
Habari za Siasa

Dk. Lwaitama: Ni uhuru wa mawazo wa wabunge Chadema

DK. Azaveli Lwaitama, Mhadhiri mstaafu
Spread the love

HATUA ya baadhi ya wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kupuuza uamuzi wa chama hicho wa kutoendelea na vikao vya Bunge, imeelezwa kuwa si tatizo bali uhuru wa mawazo. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Dk. Azaveli Lwaitama, Mhadhiri Mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akizungumza na akizungumza na MwanaHALISI Online leo tarehe 5 Mei 2020, kuhusu wabunge hao kuhudhuria vikao vya bunge kinyume na mzimamo wa chama hicho, amesema “kila mmoja ana uhuru wake, na wala sio tatizo.”

Amesema, ndani ya chama cha siasa hasa chenye misingi ya kidemokrasia, lazima utofauti na mikinzano iwepo na kwamba ndio afya ya demokrasia.

“Kutofautiana sio tatizo, kwa sababu ndio misingi ya chama chenyewe. Katika kundi la watu wengi, ni uhuru wao wa kuwaza tofauti,” amesema Dk. Lwaitama.

Miongoni mwa wabunge waliokaidi agizo hilo ni Joseph Selasini (Rombo), Anthony Komu, (Moshi Vijijini) na David Silinde (Momba) ambaye alikuwa Katibu wa Wabunge wa Chadema.

Wengine ni Peter Lijualikali (Kilombero), Jafary Michael (Moshi Mjini) na wabunge viti maalumu, Ratifa Chande, Mariam Msabaha, na Sabrina Sungura.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!