Thursday , 18 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Hussein Mwinyi ajitosa Urais Zanzibar
Habari za Siasa

Dk. Hussein Mwinyi ajitosa Urais Zanzibar

Spread the love

WAZIRI wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Dk. Hussein Mwinyi amejitosa katika kinyang’anyiro cha Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea)

Dk. Mwinyi amechukua fomu ya Urais leo Jumatano tarehe 17 Juni 2020 katika Ofisi za CCM zilizipo Ugunja Zanzibar.

Mara baada ya kukabidhiwa fomu, alikwenda eneo lililoandaliwa maalum kwa ajili ya kuzungumza na waandishi wa habari.

Dk. Mwinyi ambaye ni Mbunge wa Kwahani visiwani Zanzibar amesema, “leo sikuja kuzungumza na waandishi wa habari, nimekuja kuchukua fomu tu na wala sina la kuzungumza.”

Amesema, hajajua kilichomo kwenye hizo fomu, hivyo akaomba aende akazisome kwanza ajue kilichomo.

Dk. Mwinyi amekuwa mgombea wa tano kuchukua fomu akitanguliwa na; Mbwana Bakari Juma, Mbwana Yahya Mwinyi, Omar Sheha Mussa na Balozi Ali Karume ambaye ni Mtoto wa Rais wa kwanza wa Zanzibar, Aman Abeid Karume

Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE & MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia atua Uturuki kwa ziara ya siku 5

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumatano amewasili nchini Uturuki kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

error: Content is protected !!